Sherehe ya Hadithi za Riyadhu Swalihina باب في اليقين والتوكل 🔴 LIVE DARSA (30) Sh. Salim Issa
Darsa ilifanyika Rajab 22, 1446 H Jumatano Januari 22, 2025
باب في اليقين والتوكل
Mlango Wa Yakini Na Kutawakali
قَالَ اللهُ تَعَالَى
وَلَمَّا رَأَى الْمُؤْمِنُونَ الْأَحْزَابَ قَالُوا هَـٰذَا مَا وَعَدَنَا اللَّـهُ وَرَسُولُهُ وَصَدَقَ اللَّـهُ وَرَسُولُهُ ۚ وَمَا زَادَهُمْ إِلَّا إِيمَانًا وَتَسْلِيمًا
"Basi Waumini walipoona makundi, walisema: Haya ndio yale Aliyotuahidi Allah na Rasuli Wake, na Amesema kweli Allah na Rasuli Wake; na haikuwazidishia isipokuwa imani na kujisalimisha." Al-Ahzaab: 22.
الَّذِينَ قَالَ لَهُمُ النَّاسُ إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّـهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ﴿١٧٣
"Wale walioambiwa na watu: Hakika watu wamejumuika dhidi yenu, basi waogopeni” (Haya) Yakawazidishia imani; na wakasema: “Allah Anatutosheleza, Mzuri Alioje Mdhamini Anayetegemewa kwa yote.”
فَانقَلَبُوا بِنِعْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ وَفَضْلٍ لَّمْ يَمْسَسْهُمْ سُوءٌ وَاتَّبَعُوا رِضْوَانَ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ ذُو فَضْلٍ عَظِيمٍ ﴿١٧٤
"Basi wakarudi na neema kutoka kwa Allah na fadhila; halijawagusa ovu lolote; na wakafuatilia radhi za Allah; na Allah ni Mwenye fadhila adhimu." Aal-Imraan 3:173-174.
قَالَتْ لَهُمْ رُسُلُهُمْ إِن نَّحْنُ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَمُنُّ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۖ وَمَا كَانَ لَنَا أَن نَّأْتِيَكُم بِسُلْطَانٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١١
"Rasuli wao wakawajibu: “Sisi si chochote isipokuwa ni watu kama nyinyi, lakini Allah Anamfadhilisha Amtakaye miongoni mwa waja Wake; na haikutupasa sisi kukujieni kwa ushahidi isipokuwa kwa idhini ya Allah; na kwa Allah watawakali Waumini." Ibrahimu: 11.
فَبِمَا رَحْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ لِنتَ لَهُمْ ۖ وَلَوْ كُنتَ فَظًّا غَلِيظَ الْقَلْبِ لَانفَضُّوا مِنْ حَوْلِكَ ۖ فَاعْفُ عَنْهُمْ وَاسْتَغْفِرْ لَهُمْ وَشَاوِرْهُمْ فِي الْأَمْرِ ۖ فَإِذَا عَزَمْتَ فَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُتَوكِّلِينَ ﴿١٥٩
"Basi ni kwa rehema kutoka kwa Allah umekuwa mpole kwao (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم); na lau ungelikuwa mjeuri mwenye moyo mgumu wangelitawanyika mbali nawe (wakakukimbia); basi wasamehe na waombee maghufira na washauri katika mambo; na unapoazimia basi tawakali kwa Allah; hakika Allah Anapenda wanaotawakali." Aal-Imraan 3:159.
وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ ۚ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ بَالِغُ أَمْرِهِ ۚ قَدْ جَعَلَ اللَّـهُ لِكُلِّ شَيْءٍ قَدْرًا﴿٣﴾
Na Atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii. Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza. Hakika Allaah Anatimiza kusudio Lake. Allaah Amejaalia kwa kila kitu makadirio. [Atw-Twalaaq: 3]
إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَإِذَا تُلِيَتْ عَلَيْهِمْ آيَاتُهُ زَادَتْهُمْ إِيمَانًا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ﴿٢﴾
Hakika Waumini ni wale ambao anapotajwa Allaah nyoyo zao, zinajaa khofu na wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia iymaan, na kwa Rabb wao wanatawakali. [Al-Anfaal: 2]