top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:01:33
Darsa: سنن أبي داود 🔴 LIVE | DARSA (I) رَاوِي الحَدِيثِ : أَبُو مُوسى الأَشْعَرِيَّ Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Hijjah 01, 1447H Jumatatu Mei 18, 2026 HADITHI YA TATU Sunan Abu Daud سنن أبي داود Kitabu cha Twahara كتاب الطهارة Mlango wa Rajuli kuchagua pahala pazuri pa kukojoa باب الرَّجُلِ يَتَبَوَّأُ لِبَوْلِهِ حَدَّثَنَا مُوسَى بْنُ إِسْمَاعِيلَ، حَدَّثَنَا حَمَّادٌ، أَخْبَرَنَا أَبُو التَّيَّاحِ، حَدَّثَنِي شَيْخٌ، قَالَ لَمَّا قَدِمَ عَبْدُ اللَّهِ بْنُ عَبَّاسٍ الْبَصْرَةَ فَكَانَ يُحَدَّثُ عَنْ أَبِي مُوسَى، فَكَتَبَ عَبْدُ اللَّهِ إِلَى أَبِي مُوسَى يَسْأَلُهُ عَنْ أَشْيَاءَ، فَكَتَبَ إِلَيْهِ أَبُو مُوسَى إِنِّي كُنْتُ مَعَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَوْمٍ فَأَرَادَ أَنْ يَبُولَ فَأَتَى دَمِثًا فِي أَصْلِ جِدَارٍ فَبَالَ ثُمَّ قَالَ صلى الله عليه وسلم " إِذَا أَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يَبُولَ فَلْيَرْتَدْ لِبَوْلِهِ مَوْضِعًا " . Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1. Musa bin Ismail (Rahimahullahu) مُوسَى بْنُ إِسْمَاعِيلَ 2. Hammad (Rahimahullahu) حَمَّادٌ 3. Abut Tiyyah (Rahimahullahu) أَبُو التَّيَّاحِ 4. Shaikh (Rahimahullahu) شَيْخٌ 5. Abu Musa (Allah Awe Radhi Nae) أَبُو مُوسَى Msimulizi wa Hadithi: Abu Musa Al Ash-'ariy رَاوِي الحَدِيثِ : أَبُو مُوسى الأَشْعَرِيَّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ الاسم: عبد الله بن قيس أبو موسى الأشعري (عبد الله بن قيس بن سليم بن حضار بن حرب بن عامر بن عنز بن بكر بن عامر بن عذر بن وائل بن ناجية بن الجماهر بن الأشعر) الشهرة: عبد الله، أبو موسى الكنية: أبو موسى النسب: الأشعري, المدني، التميمي، المقرئ، اليماني بلد الإقامة: مكة، الحبشة، زبيد، عدن، البصرة، الكوفة، المدينة علاقات الراوي: أمه ظبية بنت وهب من عك، وأولاده: موسى، وإبراهيم، وأبو بردة، وأبو بكر، وأبو بردة، وحالف سعيد بن العاص، وإخوته: أبو عامر وأبو بردة وأبو رهم بنو قيس، واستعمله النبي صلى الله عليه وسلم على بعض اليمن كزبيد وعدن وأعمالهما، واستعمله عمر على البصرة والكوفة، واستعمله عثمان على الكوفة، وامرأته أم عبد الله تاريخ الوفاة: 42 هـ، أو 44 هـ، أو 50 هـ، أو 52 هـ، أو 53 هـ، ويقال 49 هـ، ويقال 51 هـ بلد الوفاة: بالكوفة أو بمكة، أو بخلف، وقيل: بالثوبة على ميلين من الكوفة بلد الرحلة: الحبشة، مكة، دمشق، المدينة طبقة رواة التقريب: صحابي مشهور الرتبة عند ابن حجر: صحابي مشهور الرتبة عند الذهبي: صحابى
Play Video
Play Video
01:11:31
Darsa: صحيح مسلم 🔴LIVE |DARSA (I) رَاوِي الحَدِيثِ: يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 30, 1447H Jumapili Mei 17, 2026 Kitabu cha Imani كتاب الإيمان باب بيان الإيمان والإسلام والإحسان ووجوب الإيمان بإثبات قدر الله سبحانه وتعالى وبيان الدليل على التبري ممن لا يؤمن بالقدر وإغلاظ القول في حقه SANAD YA TATU YA HADITHI YA Jibril عليه السلام وَحَدَّثَنِي مُحَمَّدُ بْنُ حَاتِمٍ، حَدَّثَنَا يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ، حَدَّثَنَا عُثْمَانُ بْنُ غِيَاثٍ، حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ بُرَيْدَةَ عَنْ يَحْيَى بْنِ يَعْمَرَ، وَحُمَيْدِ بْنِ عَبْدِ الرَّحْمَنِ، قَالاَ لَقِينَا عَبْدَ اللَّهِ بْنَ عُمَرَ فَذَكَرْنَا الْقَدَرَ وَمَا يَقُولُونَ فِيهِ . فَاقْتَصَّ الْحَدِيثَ كَنَحْوِ حَدِيثِهِمْ عَنْ عُمَرَ - رضى الله عنه - عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم وَفِيهِ شَىْءٌ مِنْ زِيَادَةٍ وَقَدْ نَقَصَ مِنْهُ شَيْئًا . Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1.Ishaq bin Rahwayh/Ishaaq ibn Raahawayh (Rahimahullahu) إِسْحَاقُ بْنُ إِبْرَاهِيمَ ابن راهويه 2. Qutaybah bin Said (Rahimahullahu) مُحَمَّدُ بْنُ حَاتِمٍ 3. Jariri (Rahimahullahu) يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ 4. Mansour (Rahimahullahu) عُثْمَانُ بْنُ غِيَاثٍ 5. Abu Waail (Rahimahullahu) عَبْدُ اللَّهِ بْنُ بُرَيْدَةَ 6, يَحْيَى بْنِ يَعْمَرَ 7. حُمَيْدِ بْنِ عَبْدِ الرَّحْمَنِ 8. عَبْدَ اللَّهِ بْنَ عُمَرَ 6. Omar binil Khatwaab (Allah Awe Radhi Nae) عُمَرَ - رضى الله عنه Msimulizi wa Hadithi: رَاوِي الحَدِيثِ: يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ يحيى بن سعيد بن فروخ اللقب: الأحول، الحافظ الكنية: أبو سعيد النسب: القطان، التميمي، البصري، الأحول، الحافظ بلد الإقامة: البصرة علاقات الراوي: مولى بني تميم، ابنه محمد بن يحيى بن سعيد القطان، وحفيده أحمد بن محمد تاريخ الميلاد: 120 هـ تاريخ الوفاة: 198 هـ بلد الوفاة: البصرة طبقة رواة التقريب: التاسعة الرتبة عند ابن حجر: ثقة متقن حافظ، إمام قدوة الرتبة عند الذهبي قال أحمد: ما رأيت مثله. وقال بندار: حدثنا إمام أهل زمانه يحيى القطان، واختلفت إليه عشرين سنة فما أظن أنه عصى الله قط، ولد القطان 120، ومات 198 في صفر، وكان رأسا في العلم والعمل
Play Video
Play Video
01:02:11
Majilisi: عشر ذي الحجة 🔴Majlisi ya (III) أَحْكَامُ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ وَأَيَّـامُ التَّشْرِيقِ
Majilisi ilifanyika Dhul Qa'dah 30, 1447H Jumapili Mei 17, 2026 SEHEMU YA TATU Hukumu za Siku Kumi za Dhul Hijjah na Siku za Tash-riq أَحْكَامُ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ وَأَيَّـامُ التَّشْرِيقِ Fadhila za Siku Kumi za Dhul Hijjah فَضْلُ عَشْرِ مِنْ ذِي الحِجَّةِ Fadhila za Yawmun Nahr (Siku ya Kuchinja) فضل يوم النحر Waislamu wengi hughafilika na Siku hiI adhimu Yawmun Nahr (Siku ya Kuchinja), (na hughafilika pia na) uadhama wa shani yake na utukufu wa fadhila zake nyingi na neema zake nyingi, hii ni pamoja na ukweli kwamba baadhi ya wanazuoni wanaona na kuamini kuwa Yawmun Nahr (Siku ya Kuchinja) ni siku bora zaidi ya mwaka, bila pingamizi. Ibnul Qayyim (Rahimahullahu) amesema kuwa: 'Siku bora mbele ya Allah ni Yawmun Nahr (Siku ya Kuchinja), nayo ndio Siku ya Hajjil Akbar (Hijja kubwa kabisa) kama ilivyo katika Sunan Abu Dawud (Rahimahullahu). عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ قُرْطٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ عَنِ النَّبِيِّ ﷺ قَالَ " إِنَّ أَعْظَمَ الأَيَّامِ عِنْدَ اللَّهِ تَبَارَكَ وَتَعَالَى يَوْمُ النَّحْرِ ثُمَّ يَوْمُ الْقَرِّ " . Kutokana na Abdullah bin Qurtwin (Allah Awe Radhi Nae) kutokana na Nabii ﷺ amesema: “Hakika Siku ziliyo bora (tukufu) kabisa kwa Allah (Tabaaraka wa Ta'alaa) ni Yawmun Nahr (Siku ya kuchinja), kisha Yawmul Qarri.” Na Yawmul Qarri ni ile siku ya kutulia Mina, nayo ni siku ya kumi na moja. Na pamemwa kuwa: Yawmu Arafah (Siku ya Arafa) ni bora kuliko hiyo (yaani: Yawmun Nahr), kwa kuwa Saumu yake inafidia (dhambi za) miaka miwili, na hakuna siku ambayo ndani yake Allah Anayoacha kwa wingi huru waja kutokana na Moto (wale waliostahiki kuingia Motoni) zaidi kuliko Yawmu Arafah (Siku ya Arafa), na kwamba Yeye (Subhaanahu wa Ta'alaa) katika (siku hiyo) Huwa karibu, kisha Hujigamba (yaani: kuhusu Ahali wa Kisimamo cha Arafah) kwa Malaika Wake. Na kauli ya kwanza ndio sahihi; kwa kuwa Hadithi inadalilisha na kuthibitisha hilo na haipingwi na chochote. Na ni sawasawa kama ikiwa Yawmun Nahr (Siku ya kuchinja) ndio siku bora au Yawmu Arafah (Siku ya Arafa ndio bora); kinachotakiwa na kutakikana kwa Muislamu -awe ni hajji (mwenye kuhiji) au mkaazi- kuwa mwangalifu ili apate kuweza kufikia kudiriki na kutambua fadhila zake na kuichangamkia fursa yake. ا Baadhi ya Hukumu za Udh hiyyah na Kuamrisha Kwake بعض أحكام الأضحية ومشروعيته Lililoasili kuhusu Udh hiyyah (kuchinja) ni kuwa ni haki waliyowekewa wale waliohai, kama alivyokuwa akifanya Rasuli wa Allah ﷺ na Swahaba zake (Allah Awe Radhi Nao Jamia); walikuwa wakichinjia nafsi zao na ahali zao, ama kile ambacho baadhi ya watu wa kawaida (yaani: wasio kuwa na elimu) wanachodhania na kufikiria kuwa Udh hiyyah (kuchinja) ni mahususi kwa wafu, basi (ni vyema tuelewe kuwa) hili halina msingi wowote ule katika Dini. Udh hiyyah kwa niaba ya kuwachinjia wafu imegawanywa katika vigawanyo vitatu: Cha kwanza: Kuwachinjia wafu kwa niaba yao kwa kuwajumuisha na waliohai, mfano mtu anajichinjia (nafsi yake) na (hapohapo) anachinjia ahali baiti yake, na katika dhamira yake (anakusudia) kuwajumuisha waliohai na wafu, na asili ya hii ni uchinjaji wa Nabii ﷺ kwa nafsi yake na ahali baiti yake na miongoni mwao walikuwemo waliokuwa wameshakufa kabla. Cha pili: Kuwachinjia wafu kwa ajili ya kutekekeza wasia wao. Na asili ya hii ni Kauli Yake Ta’alaa: ﴾ فَمَن بَدَّلَهُ بَعْدَ مَا سَمِعَهُ فَإِنَّمَا إِثْمُهُ عَلَى الَّذِينَ يُبَدِّلُونَهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ ﴿١٨١ "Atakayeubadilisha (wasia) baada ya kuusikia, basi hakika dhambi yake ni juu ya wale watakaoubadilisha; hakika Allah ni Samiy'un (Mwenye Kusikia yote) Alimu." Cha tatu: Kuwachinjia wafu pekee (bila ya kuwajumuisha na waliohai) kwa kujitolea, hii inajuzu. Na Fuqahaa wa dhehebu la Kihanbali wameeleza kuwa thawabu zake zinamfikia maiti na ananufaika nazo (kauli yao hii inaegemezwa na) Qiyaas ya kumtolea (maiti) sadaka kwa niaba yake, lakini hatuoni (usahihi wa) kumchinjia maiti mahususi (hususan bila ya kumjumuisha na waliohai) ni katika Sunnah, kwa kuwa Nabiiﷺ hakumchinjia mmoja yeyote yule mahususi (hususan bila ya kumjumuisha na waliohai) katika maiti zake, Nabiiﷺ hakumchinjia ami yake Hamza (Allah Awe Radhi Nae), ambaye alikuwa mmoja wa jamaa zake wa karibu na kipenzi, na wala (hakuwachinjia) mahususi (hususan bila ya kuwajumuisha na waliohai) waladi zake ambao walikufa wakati wa uhai wakeﷺ, ambao ni mabanati watatu waliokuwa wamekwishaolewa (Allah Awe Radhi Nao Jamia) na wala (hakumchinjia) zaujiti wake Khadija (Allah Awe Radhi Nae), ambaye ndie kipenzi zaidi katika wake zake wote (Allah Awe Radhi Nao Jamia), na wala haikupokelewa kutokana na Swahaba (Allah Awe Radhi Nao Jamia) katika zama zake ﷺ kwamba mmoja yeyote yule aliwahi kumchinjia yeyote yule katika maiti zake.
Play Video
Play Video
01:04:28
Darsa: حق الأولاد على الوالدين 🔴 LIVE | DARSA Haki za Watoto Juu ya Wazazi (III) Ust. Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 30, 1447H Jumapili Mei 17, 2026 SEHEMU YA TATU Haki za Watoto Juu ya Wazazi Wawili حق الأولاد على الوالدين Kwa hakika Allah سبحانه Atamuuliza mzazi kuhusu waladi wake Siku ya Qiyamah, kabla ya kumuuliza walad kuhusu baba ake, kwani kama vile baba alivyo na haki juu ya waladi wake, basi pia walad naye ana haki juu ya baba yake; kama Alivyosema Allah تعالى: ﴾وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا ۖ وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا ۚ إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٨ "Na Tumemuusia Insani -binadamu- kuwafanyia wema wazazi wake wawili; lakini wakikushikilia kuwa unishirikishe na ambayo huna ilimu nayo, basi usiwatii; Kwangu ni marejeo yenu, Nitakujulisheni yale mliyokuwa mkiyatenda." [Al Ankabut 29:8] Pia Amesema Allah تعالى: يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا قُوا أَنفُسَكُمْ وَأَهْلِيكُمْ نَارًا وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ ﴾عَلَيْهَا مَلَائِكَةٌ غِلَاظٌ شِدَادٌ لَّا يَعْصُونَ اللَّـهَ مَا أَمَرَهُمْ وَيَفْعَلُونَ مَا يُؤْمَرُونَ﴿٦ "Enyi mlioamini! Jikingeni nafsi zenu pamoja na ahli zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe; wanaulinda Malaika washupavu wasio na huruma, shadidi, hawamuasi Allah kwa yale Anayowaamrisha na wanafanya yale wanayoamrishwa." [At Tah-rim 66:6] Basi usia/wasia wa Allah kwa wazazi kuhusu waladi wao umetangulia na wasia wa waladi kwa baba zao, hivyo basi yeyote yule atayepuuza na kuzemnbea kumfundisha waladi wake kile kitakachoweza kumnufaisha na kumwacha ajiamulie mwenyewe, huyo atakuwa amefanya kosa kubwa. Na kwa hakika kufisidika kwa watoto wengi huja kwa kule wazazi wao kupuuza na kushindwa kuwafundisha mambo ya lazima ya Dini yao na Sunnah zake. Waliwapuuza katika utotoni mwao, kwa hivyo hawakuwa na manufaa kwa wazazi wao katika uzee wao. Utangulizi unaohusiana na haki za walad مقدمات متعلقة بحق الولد .الولد أمانة سيسأل عنها الوالدان يوم القيامة Walad ni amana ambayo wazazi watawajibika kwayo Siku ya Qiyaamah :عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ "الرَّجُلُ رَاعٍ عَلَى أَهْلِ بَيْتِهِ وَهْوَ مَسْئُولٌ عَنْهُمْ، وَالْمَرْأَةُ رَاعِيَةٌ عَلَى بَيْتِ بَعْلِهَا وَوَلَدِهِ وَهْىَ مَسْئُولَةٌ عَنْهُمْ... ". Amesema Rasuli a Allah صلى الله عليه وسلم: "Rajuli -mume- ni mchungaji wa ahali wake -familia yake-, naye ataulizwa juu ya anaowachunga; na mwanamke -mke- ni mchungaji wa nyumba ya mumewe, naye (pia) ataulizwa juu ya anachokichunga.” [Wamewafikiana Bukhari na Muslim]. Usia/wasia kwa wazazi kuhusu watoto wao unatangulia usia wa watoto kuhusu wazazi wao. مسؤولية تربية الأبناء ورعايتهم تقع على الوالدين في المقام الأول Jukumu la kulea na kuwatunza watoto huwa liko juu ya wazazi hasa. الوالدان أشد الناس تأثيراً فيما يكون عليه الأولاد في المستقبل Wazazi ndio watu wenye ushawishi mkubwa katika kuutengeneza na kuuelekeza mustakabali wa watoto wao. :عَنِ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " مَا مِنْ مَوْلُودٍ إِلاَّ يُولَدُ عَلَى الْفِطْرَةِ، فَأَبَوَاهُ يُهَوِّدَانِهِ أَوْ يُنَصِّرَانِهِ أَوْ يُمَجِّسَانِهِ " Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه) kuwa: Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Hakuna kizazi kinachozaliwa (mtoto mchanga) isipokuwa anazaliwa katika 'fitwrah' kisha wazazi wake (humbadilisha na) humuingiza katika Uyahudi, au Unasara au Umajusi..." [Wamewafikiana Bukhari na Muslim] Haki za watoto juu ya wazazi wao ni za aina mbili حقوق الأولاد على الآباء قسمان Haki Ya Kwanza: Kabla ya Kuzaliwa الأول: قبل وجود الولد Haki Ya Pili: Baada ya Kuzaliwa الثاني: بعد وجود الولد Haki Ya Pili: Baada ya Kuzaliwa الثاني: بعد وجود الولد *Kuomba dua kutengenea kwa walad دعاء الله بصلاح الولد * Kumpa -kumwita- walad jina zuri تسمية الولد باسم حسن *Kumhurumia na kuwa na upole katika muamala nae رحمته والرفق به في التعامل *Kulinda heshima yake na kuepuka kumtusi, kumuumbua, na kumpiga الحفاظ على كرامته وتجنب سبه وتعنيفه وضربه *Kuchunga haki yake ya kucheza na kucheza naye kwa njia itayomfaidisha na wala haitomuudhi مراعاة حقه في اللعب واللعب معه بما يفيده ولا يؤذيه *Kuwa na pupa juu ya kumfunza walad na kumuadabisha الحرص على تعليم الولد وتأديبه *Kuwa na pupa -hamu- yakumfunza itikadi sahihi الحرص على تعليمه العقيدة السليمة *Kuwa na pupa ya kumfundisha Qur-aani utoto mwake الحرص على تعليمه القرآن في صغره *Kuwa na pupa ya kumfunza Faraadh za Dini, Halali na Haramu utotoni mwake
Play Video
Play Video
01:14:32
Majilisi: عشر ذي الحجة 🔴Majlisi ya (II) أَحْكَامُ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ وَأَيَّـامُ التَّشْرِيقِ
Majilisi ilifanyika Dhul Qa'dah 29, 1447H Jumamosi Mei 16, 2026 SEHEMU YA PILI Hukumu za Siku Kumi za Dhul Hijjah na Siku za Tash-riq أَحْكَامُ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ وَأَيَّـامُ التَّشْرِيقِ Fadhila za Siku Kumi za Dhul Hijjah فَضْلُ عَشْرِ مِنْ ذِي الحِجَّةِ مَا يَجْتَنِبْهُ فِي العَشْرِ مَنْ أَرَادَ الأٌضْحِيَّةَ Anayopaswa kujiepusha nayo katika Siku Kumi Mwenye kutaka -kuazimia- Kuchinja Yale Anayotakiwa Kujiepusha Nayo Mwenye Kutaka Kuchinja فيما يجتنبه من أراد الأضحية Mwenye kudhamiria kuchinja na ikawa shahari ya Dhul Hijjah umeingia: ima kwa kuona hilali au kukamilisha siku thelathini za Dhul Qa'dah basi ni haitakikani (Sh. katumia tamshi: haramu) kwake kunyoa (kukata) chochote kile katika nywele zake au kuchuna ngozi ya mwili wake mpaka achinje kichinjo chake, kutokana na Hadithi ya Ummu Salamah عَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رضي الله عنها أَنَّ النَّبِيَّ ﷺ قَالَ :" إِذَا رَأَيْتُمْ هِلاَلَ ذِي الْحِجَّةِ وَأَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يُضَحِّيَ فَلْيُمْسِكْ عَنْ شَعْرِهِ وَأَظْفَارِهِ Kutokana na Ummu Salamah (Allah Awe Radhi Nae) kwamba Nabii ﷺ amesema: “Mtakapouona mwezi wa Dhul Hijjah na mmoja wenu akadhamiria kuchinja, basi ajizuie (kukata) nywele zake na kucha zake.” Na katika riwayah: " فَلاَ يَأْخُذَنَّ مِنْ شَعْرِهِ وَلاَ مِنْ أَظْفَارِهِ شَيْئًا حَتَّى يُضَحِّيَ " . “Basi asiguse (asikata) chochote kile katika nywele zake na wala katika kucha zake mpaka atakapochinja.” Na kama atadhamiria kuchinja katika siku kumi (mfano siku pili au ya tatu na kadhallika), basi atatakiwa ajiepushe (na hayo yaliyokatazwa) kuanzia pale alipodhamiria, na hakuna dhambi kama atakuwa amekata (nywele au kucha) kabla ya huko kudhamiria kwake. Hekima katika katazo hili والحكمة في هذا النَّهي Ni kuwa: pale mwenye kuchinja aliposhirikiana na mwenye kuhiji katika baadhi ya amali za ibada ya Hijjah, ambazo ni (miongoni mwa amali za) kujikurubisha kwa Allah kwa kule kuchinja kwake kichinjo, basi hushirikiana nae (pia) katika baadhi ya sifa maalumu za Ihramu katika kujizuia (kukata) nywele na mfano wa hayo, na hivyo basi inajuzu kwa ahali wa mwenye kuchinja (yaani: sio mchinjaji mwenyewe) kukata nywele zao, kucha zao na kuchukua chochote kile katika miili yao katika hizo siku kumi. * Hukumu hii (ya kujizuia kukata nywele na mfano wake) ni mahususi kwa yule anayechinja, ama yule anayechinjiwa (ahali wa mchinjaji na kadhalika) huwa haimhusu; kwa kuwa Nabii ﷺ kasema: "وَأَرَادَ أَحَدُكُمْ أَنْ يُضَحِّيَ. " "Na mmoja wenu akadhamiria kuchinja ...” na wala hakusema au anayechinjiwa (ahali wa mchinjaji na kadhalika); na kwa sababu Nabii ﷺ alikuwa akichinja kwa niaba ya ahali zake, na haikupokelewa kutokana nae ﷺ kwamba aliwaamrisha (ahali zake) kujizuia (kukata) nywele na mfano wa hayo. * Na mwenye kudhamiria kuchinja akikata chochote kile katika nywele zake, au kucha zake au mwili wake, basi ni lazima atubie kwa Allah, na wala asirudie (asifanye tena), na wala hana kafara, na hilo halimzuii kuchinja kama wanavyodhania baadhi ya watu wa kawaida. * Na pale atakapokata chochote kile katika hayo hali ya kusahau au kutojua, au nywele zimedondoka (anguka) bila kukusudia, basi hakuna dhambi juu yake, na wakati wowote ule akihitaji kukata (nywele zake na mfano wa hayo) basi anaweza kukata, na wala hakuna ubaya wowote ule juu yake, mfano kucha yake imekatika na inamuudhi (inamuumiza) basi anaweza kuukata, au nywele zinamuudhi (zinashuka na kuingia) machoni mwake, basi anaweza kuzikata, au anahitaji kuzikata kwa gharadhi ya kutibu jeraha na kadhalika.
Play Video
Play Video
51:38
Majilisi: عشر ذي الحجة 🔴 Majilisi ya (I) أَحْكَامُ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ وَأَيَّـامُ التَّشْرِيقِ
Majilisi ilifanyika Dhul Qa'dah 28, 1447H Ijumaa Mei 15, 2026 SEHEMU YA KWANZA Hukumu za Siku Kumi za Dhul Hijjah na Siku za Tash-riq أَحْكَامُ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ وَأَيَّـامُ التَّشْرِيقِ Fadhila za Siku Kumi za Dhul Hijjah فَضْلُ عَشْرِ مِنْ ذِي الحِجَّةِ Masiku kumi ya mwanzo ya Shahari ya Dhul-Hijjah yana fadhila nyingi, na amali yoyote ile njema itendayo ndani yake huwa inapendeza mno mbele ya Allah. :عن ابن عباس رضي الله عنهما أن النبي صلى الله عليه وسلم قال ((مَا مِنْ أَيَّامٍ الْعَمَلُ الصَّالِحُ فِيهَا أَحَبُّ إِلَى اللَّهِ مِنْ هَذِهِ الْأَيَّامِ)) يَعْنِي أَيَّامَ الْعَشْرِ قَاُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَلَا الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ؟ "قَالَ: "وَلَا الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ إِلَّا رَجُلٌ خَرَجَ بِنَفْسِهِ وَمَالِهِ فَلَمْ يَرْجِعْ مِنْ ذَلِكَ بِشَيْ Kutokana na Ibn Abbas (Allah Awe Radhi Nao) kwamba Nabii صلى الله عليه وسلم : “Hakuna siku ambazo amali njema zinazotendwa humo huwa zinapendwa mno na Allah kama (amali zinazotendwa katika) siku kumi hizi.” Yaani: Siku kumi za mwanzo za Dhul Hijjah. (Swahaba Allah Awe Radhi Nao Jamia) Wakauliza kwa kusema: 'Ewe Rasuli wa Allah! Hata kuliko Jihadi katika Sabili ya Allah? Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم akawajibu kwa kusema: “Ndio! Hata Jihadi katika Sabili ya Allah; isipokuwa mtu aliyetoka (kwenda Jihadi) kwa nafsi yake na mali yake kisha kisirudi chochote kile katika hivyo.” Miongoni mwa fadhila za masiku kumi haya ni kuwa: I. Allah Ameziapia Siku Kumi hizi: "وَالْفَجْرِ. وَلَيَالٍ عَشْرٍ" "Naapa kwa Alfajiri. Na kwa masiku kumi" [Al-Fajr: 1-2] Wanazuoni wa tafsiri wamekubaliana kwamba masiku yaliyokusudiwa hapo ni masiku kumi ya mwanzo ya Shahari ya Dhul-Hijjah. 2. Siku za manufaa na dhikr (kumdhukuru Allah) kathira (kwa wingi): "لِيَشْهَدُوا مَنَافِعَ لَهُمْ وَيَذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ فِي أَيَّامٍ مَّعْلُومَاتٍ" "Ili washuhudie manufaa yao na kulitaja Jina la Allah katika siku zinazojulikana" [Al-Hajj: 28] 3. Karibu ibada zote zinajumuika katika masiku haya: * Sala * Kufunga (siku hizi hususan siku ya Arafah) * Utekelezaji wa ibada ya (Umrah) na Hijjah) *Ibada ya Kuchinja *Kumdhukuru Allah kwa wingi hasahasa uletaji wa Tak-bira ambazo ziko za namna mbili: 1. Al-Mutwlaq (zisizokuwa na nyakati maalumu) Tak-bira za wakati wote mchana na usiku, mahali popote ulipo (ghairi chooni), tokea unapoingia mwezi wa Dhul-Hijjah na inaendelea hadi siku ya mwisho ya Tashriqi (tarehe 13 Dhul-Hijjah) na kumalizika baada ya kuingia Maghribi. 2. Al-Muqayyad (zilizodhibitiwa/fungwa kwa wakati na pahali mahususi) Hizi ni zile Tak-bir zinazotakiwa kuletwa kila baada ya Sala ya faradhi na huanza baada ya Sala ya Alfajiri Siku ya Arafah hadi Sala ya Alasiri siku ya mwisho ya Tashriqi. اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، وَلِلَّهِ الْحَمْد Allahu Ak-bar, Allahu Ak-bar, laa Ilaha illa Allah, Allahu Ak-bar Allahu Ak-bar walillahil-hamd.
Play Video
Play Video
01:15:28
DARSA: مَوْسُوعَة عُلُومِ الحَدِيْثِ وفُنُونِه 🔴 LIVE| DARSA: ljaza إِجَازَة Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Qa'dah 28, 1447H Ijumaa Mei 15, 2026
Play Video
Play Video
59:48
Majilisi: فَضْلُ عَشْرِ ذِي الحِجَّةِ 🔴LIVE | Fadhila za Siku Kumi za Dhul Hijjah Ust Salim Khatib
Majilisi ilifanyika Dhul Qa'dah 28, 1447H Ijumaa Mei 15, 2026 Fadhila za Siku Kumi za Dhul Hijjah فضل عشر ذي الحجة Masiku kumi ya mwanzo ya Shahari ya Dhul-Hijjah yana fadhila nyingi, na amali yoyote ile njema itendayo ndani yake huwa inapendeza mno mbele ya Allah. :عن ابن عباس رضي الله عنهما أن النبي صلى الله عليه وسلم قال ((مَا مِنْ أَيَّامٍ الْعَمَلُ الصَّالِحُ فِيهَا أَحَبُّ إِلَى اللَّهِ مِنْ هَذِهِ الْأَيَّامِ)) يَعْنِي أَيَّامَ الْعَشْرِ قَاُوا: يَا رَسُولَ اللَّهِ وَلَا الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ؟ "قَالَ: "وَلَا الْجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللَّهِ إِلَّا رَجُلٌ خَرَجَ بِنَفْسِهِ وَمَالِهِ فَلَمْ يَرْجِعْ مِنْ ذَلِكَ بِشَيْ Kutokana na Ibn Abbas (Allah Awe Radhi Nao) kwamba Nabii صلى الله عليه وسلم : “Hakuna siku ambazo amali njema zinazotendwa humo huwa zinapendwa mno na Allah kama (amali zinazotendwa katika) siku kumi hizi.” Yaani: Siku kumi za mwanzo za Dhul Hijjah. (Swahaba Allah Awe Radhi Nao Jamia) Wakauliza kwa kusema: 'Ewe Rasuli wa Allah! Hata kuliko Jihadi katika Sabili ya Allah? Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم akawajibu kwa kusema: “Ndio! Hata Jihadi katika Sabili ya Allah; isipokuwa mtu aliyetoka (kwenda Jihadi) kwa nafsi yake na mali yake kisha kisirudi chochote kile katika hivyo.” Miongoni mwa fadhila za masiku kumi haya ni kuwa: I. Allah Ameziapia Siku Kumi hizi: "وَالْفَجْرِ. وَلَيَالٍ عَشْرٍ" "Naapa kwa Alfajiri. Na kwa masiku kumi" [Al-Fajr: 1-2] Wanazuoni wa tafsiri wamekubaliana kwamba masiku yaliyokusudiwa hapo ni masiku kumi ya mwanzo ya Shahari ya Dhul-Hijjah. 2. Siku za manufaa na dhikr (kumdhukuru Allah) kathira (kwa wingi): "لِيَشْهَدُوا مَنَافِعَ لَهُمْ وَيَذْكُرُوا اسْمَ اللَّهِ فِي أَيَّامٍ مَّعْلُومَاتٍ" "Ili washuhudie manufaa yao na kulitaja Jina la Allah katika siku zinazojulikana" [Al-Hajj: 28] 3. Karibu ibada zote zinajumuika katika masiku haya: * Sala * Kufunga (siku hizi hususan siku ya Arafah) * Utekelezaji wa ibada ya (Umrah) na Hijjah) *Ibada ya Kuchinja *Kumdhukuru Allah kwa wingi hasahasa uletaji wa Tak-bira ambazo ziko za namna mbili: 1. Al-Mutwlaq (zisizokuwa na nyakati maalumu) Tak-bira za wakati wote mchana na usiku, mahali popote ulipo (ghairi chooni), tokea unapoingia mwezi wa Dhul-Hijjah na inaendelea hadi siku ya mwisho ya Tashriqi (tarehe 13 Dhul-Hijjah) na kumalizika baada ya kuingia Maghribi. 2. Al-Muqayyad (zilizodhibitiwa/fungwa kwa wakati na pahali mahususi) Hizi ni zile Tak-bir zinazotakiwa kuletwa kila baada ya Sala ya faradhi na huanza baada ya Sala ya Alfajiri Siku ya Arafah hadi Sala ya Alasiri siku ya mwisho ya Tashriqi. اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، وَلِلَّهِ الْحَمْد Allahu Ak-bar, Allahu Ak-bar, laa Ilaha illa Allah, Allahu Ak-bar Allahu Ak-bar walillahil-hamd.
Contact
bottom of page