top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
03:03
Darsa na Mihadhara's Personal Meeting Room
Play Video
Play Video
51:04
Darsa ya Tafsiri: شرح المصباح المنير في تهذيب تفسير ابن الكثير 🔴LIVE Aayah 174 -176 Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Hijjah 22, 1447H Jumatatu Juni 08, 2026 Tafsiri/Tarjama ya Suratul Baqarah تفسير سورة البقرة Kulaumu Mayahudi kwa kule kuficha kwao kile Alichokiteremsha Allah ذَمُّ اليَهُودِ عَلَى كِتْمَانِهِم مَاأَنْزَلَ اللهُ إِنَّ الَّذِينَ يَكْتُمُونَ مَا أَنزَلَ اللَّـهُ مِنَ الْكِتَابِ وَيَشْتَرُونَ بِهِ ثَمَنًا قَلِيلًا ۙ أُولَـٰئِكَ مَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ إِلَّا النَّارَ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ اللَّـهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ﴾وَلَا يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿١٧٤ "Hakika wale wanaoficha yale Aliyoyateremsha Allah katika Kitabu na wakakibadilisha kwa thamani ndogo, hao hawali katika matumbo yao isipokuwa Moto, na wala Allah Hatowasemesha Siku ya Qiyaamah na wala Hatowatakasa, nao watapata adhabu iumizayo." [Al Baqarah 2:174] ﴾أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ اشْتَرَوُا الضَّلَالَةَ بِالْهُدَىٰ وَالْعَذَابَ بِالْمَغْفِرَةِ ۚ فَمَا أَصْبَرَهُمْ عَلَى النَّارِ ﴿١٧٥ "Hao ndio wale waliobadilisha dhalala -upotofu- badala ya uongofu, na adhabu kwa maghufira; basi kuvumilia gani huko kwao ndani ya Moto?! [Al Baqarah 2:175] ﴾ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّـهَ نَزَّلَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ ۗ وَإِنَّ الَّذِينَ اخْتَلَفُوا فِي الْكِتَابِ لَفِي شِقَاقٍ بَعِيدٍ ﴿١٧٦ "Hayo ni kwa sababu Allah Amekiteremsha Kitabu kwa haki; na hakika wale waliohitilafiana katika Kitabu wamo katika upinzani wa mbali." [Al Baqarah 2:176]
Play Video
Play Video
54:21
Darsa: صحيح مسلم 🔴LIV |DARSA (III) رَاوِي الحَدِيثِ: يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Hijjah 21, 1447H Jumapili Juni 07, 2026 Kitabu cha Imani كتاب الإيمان باب بيان الإيمان والإسلام والإحسان ووجوب الإيمان بإثبات قدر الله سبحانه وتعالى وبيان الدليل على التبري ممن لا يؤمن بالقدر وإغلاظ القول في حقه SANAD YA TATU YA HADITHI YA Jibril عليه السلام وَحَدَّثَنِي مُحَمَّدُ بْنُ حَاتِمٍ، حَدَّثَنَا يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ، حَدَّثَنَا عُثْمَانُ بْنُ غِيَاثٍ، حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ بُرَيْدَةَ عَنْ يَحْيَى بْنِ يَعْمَرَ، وَحُمَيْدِ بْنِ عَبْدِ الرَّحْمَنِ، قَالاَ لَقِينَا عَبْدَ اللَّهِ بْنَ عُمَرَ فَذَكَرْنَا الْقَدَرَ وَمَا يَقُولُونَ فِيهِ . فَاقْتَصَّ الْحَدِيثَ كَنَحْوِ حَدِيثِهِمْ عَنْ عُمَرَ - رضى الله عنه - عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم وَفِيهِ شَىْءٌ مِنْ زِيَادَةٍ وَقَدْ نَقَصَ مِنْهُ شَيْئًا . Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1.Ishaq bin Rahwayh/Ishaaq ibn Raahawayh (Rahimahullahu) إِسْحَاقُ بْنُ إِبْرَاهِيمَ ابن راهويه 2. Qutaybah bin Said (Rahimahullahu) مُحَمَّدُ بْنُ حَاتِمٍ 3. Jariri (Rahimahullahu) يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ 4. Mansour (Rahimahullahu) عُثْمَانُ بْنُ غِيَاثٍ 5. Abu Waail (Rahimahullahu) عَبْدُ اللَّهِ بْنُ بُرَيْدَةَ 6, Yahya bin Ya;mar (Rahimahullau) يَحْيَى بْنِ يَعْمَرَ 7. Humaydi bin Abdur Rahman (Rahimahullahu) حُمَيْدِ بْنِ عَبْدِ الرَّحْمَنِ 8. Abdullahi bin Omar (Allah Awe Radhi Nao) عَبْدَ اللَّهِ بْنَ عُمَرَ 6. Omar binil Khatwaab (Allah Awe Radhi Nae) عُمَرَ - رضى الله عنه Msimulizi wa Hadithi: Yahya bin Said Al Qatwani رَاوِي الحَدِيثِ: يَحْيَى بْنُ سَعِيدٍ الْقَطَّانُ يحيى بن سعيد بن فروخ اللقب: الأحول، الحافظ الكنية: أبو سعيد النسب: القطان، التميمي، البصري، الأحول، الحافظ بلد الإقامة: البصرة علاقات الراوي: مولى بني تميم، ابنه محمد بن يحيى بن سعيد القطان، وحفيده أحمد بن محمد تاريخ الميلاد: 120 هـ تاريخ الوفاة: 198 هـ بلد الوفاة: البصرة طبقة رواة التقريب: التاسعة الرتبة عند ابن حجر: ثقة متقن حافظ، إمام قدوة الرتبة عند الذهبي قال أحمد: ما رأيت مثله. وقال بندار: حدثنا إمام أهل زمانه يحيى القطان، واختلفت إليه عشرين سنة فما أظن أنه عصى الله قط، ولد القطان 120، ومات 198 في صفر، وكان رأسا في العلم والعمل
Play Video
Play Video
50:10
Darsa: حُقُوقُ الزَّوْجَيْنِ 🔴 LIVE | DARSA Haki za Wanandoa Wawili (I) Ust. Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Hijjah 21, 1447H Jumapili Juni 07, 2026 SEHEMU YA KWANZA Haki za Wanandoa Wawili حُقُوقُ الزَّوْجَيْنِ Uislamu unasisitiza umuhimu wa uhusiano madhubuti na wenye nguvu na mshikamano baina ya wanandoa wawili; kwa minajili hiyo ndio Allah Akauita ' ahadi iliyo madhubut مِّيثَاقًا غَلِيظًا ' na Akajaalia baina ya wanandoa wawili mawada -mapenzi- na rahmah. Pia Uislamu umeweka suluhisho la kivitendo lenye lengo la kuweza kuhakikisha na kudhamini uendeleaji wa maisha ya ndoa, na huku ukibughudhi aina yoyote ile itayoweza kuwa ni sababu ya kutengana kwa wanandoa wawili kwa sabili yoyote ile, na ikiwa ni pamoja na talaka, kwa kuifanya kuwa ni suluhisho la mwisho. Na ili kuhakikisha mwendelezo wa maisha ya kindoa; Allah عَزَّوَجَلَّ na Rasuli Wake صلى الله عليه وسلم wameweka haki kwa kila mwenzi na wajibu kwa kila mmoja kwa mwenzake. Kadiri wanavyotimiza wajibu wao, ndivyo maisha yao ya kindoa yatakavyonyooka na kuwa yenye mshikamano zaidi. Haki za Mume Juu ya Mke حُقُوقُ الزَّوْجِ عَلَى الزَّوْجَةِ * حق الزوج على زوجته من أعظم الحقوق بعد حق الله عليها Haki za mume juu ya mkewe ni miongoni mwa haki kubwa zaidi baada ya haki za Allah juu ya mke. * جعل الله القوامة للرجل على المرأة وفضله عليها Allah عَزَّوَجَلَّ Amejaalia usimamizi wa mwanamke kwa rajuli -mume- na Amemfadhilisha mwanamume kuliko mwanamke. *طاعة الزوج والقيام بحقوقه يقدم على طاعة الوالدين والقيام بحقوقهما Kumtii mume na kule kutekeleza haki zake kunatangulizwa -kunakadimishwa- mbele ya kuwatii wazazi wawili na kule kutekeleza -kusimamia- haki zao. * Kutimiza haki za mume ni tariki -njia- ya kutimiza haki za Allah أداء حق الزوج طريق لأداء حق الله عزوجل *Kutimiza haki za mume ni katika sababu ya kuingia Jannah أداء حق الزوج من أسباب دخول الجنة * يجب على الزوجة تلبية حق الزوج في الفراش، مالم يكن ضررتعذر به Ni wajibu juu ya mke kutimiza haki za mume ya mahusiano ya kindoa, madamu hakuna madhara ambayo kwayo atatolea udhuru. *Kubaki nyumbani kwake na asitoke bila idhini ya mumewe لزوم بيتها فلا تخرج بغير إذن زوجها *Kutofunga funga za Sunnah -za kujitolea- bila idhini ya mumewe عدم التطوع بالصوم إلا بإذن زوجها *Kujihifadhi katika hali ya kutokuweko mumewe حفظ غيبة زوجها *Kuhifadhi nafsi yake kwa kutochanganyika na wasiokuwa maharamu zake bila ya haja, na bila ya idhini ya mumewe. حفظ نفسها عن مخالطة الأجانب لغير حاجة، وبإذن زوجها
Play Video
Play Video
01:02:49
Darsa: صحيح البخاري 🔴 LIVE | DARSA (X) رَاوِي الحَدِيثِ : مالك بن أنس Ust Abu Raifah
Darsa ilifanyika Dhul Hijjah 20, 1447H Jumamosi Juni 06, 2026 باب كَيْفَ كَانَ بَدْءُ الْوَحْىِ إِلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم Mlango: Namna ya Wahyi Ulivyoanza kwa Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) HADITHI YA PILI حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، قَالَ أَخْبَرَنَا مَالِكٌ، عَنْ هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ ـ رضى الله عنها ـ أَنَّ الْحَارِثَ بْنَ هِشَامٍ ـ رضى الله عنه ـ سَأَلَ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ كَيْفَ يَأْتِيكَ الْوَحْىُ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " أَحْيَانًا يَأْتِينِي مِثْلَ صَلْصَلَةِ الْجَرَسِ ـ وَهُوَ أَشَدُّهُ عَلَىَّ ـ فَيُفْصَمُ عَنِّي وَقَدْ وَعَيْتُ عَنْهُ مَا قَال وَأَحْيَانًا يَتَمَثَّلُ لِيَ الْمَلَكُ رَجُلاً فَيُكَلِّمُنِي فَأَعِي مَا يَقُولُ ". قَالَتْ عَائِشَةُ رضى الله عنها وَلَقَدْ رَأَيْتُهُ يَنْزِلُ عَلَيْهِ الْوَحْىُ فِي الْيَوْمِ الشَّدِيدِ الْبَرْدِ، فَيَفْصِمُ عَنْهُ وَإِنَّ جَبِينَهُ لَيَتَفَصَّدُ عَرَقًا. Ametuhadithia Abdullahi bin Yusuf, amesema: ametupasha habari Malik kutokana na Hishami bin 'Urwah kutokana na baba ake, kutokana na Aishah Mama wa Waumini (رضي الله عنها) kwamba: Al-Harith bin Hisham (رضي الله عنه) alimuuliza Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa kusema: 'Ewe Rasuli wa Allah! Vipi unakujia Wahyi?” Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamjibu kwa kusema: “Wakati mwengine unanijia kama sauti ya kengele, aina hii ya Wahyi ni shadidi -ngumu- zaidi kwangu kuliko zote na kisha hali hiyo hunipitia baada ya kuwa nimeshafahamu kile nilichofunuliwa; wakati mwingine Malaika huja katika umbile la rajuli, hunisemresha na kuyaelewa anayosema.” Aaishah (رضي الله عنها) amesema: 'Kwa hakika nilimwona (Rasuli wa Allah صلى الله عليه وآله وسلم) akiletewa Wahyi siku ya baridi kali na akaona jasho likimdondoka usoni (baada ya kumalizika Wahyi). Wapokezi wa Hadithi hii رُوَاةُ هَذَا الحَدِيثِ 1. Abdullahi bin Yusuf (Rahimahullahu) عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ 2. Malik bin Anas bin Malik (Rahimahullahu) مالك بن أنس بن مالك 3. Hishami bin 'Urwah (Rahimahullahu) هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ 4. 'Urwah bin Az Zubair (Rahimahullahu) عُرْوَةَ بنِ الزُّبَيْرِ بنِ العَوَّامِ 5. Aishah Ummul Muminina (Allah Awe Radhi Nae) عَائِشَةَ أُمِّ الْمُؤْمِنِينَ ـ رضى الله عنها Msimulizi wa Hadithi: Malik bin Anas bin Malik مالك بن أنس بن مالك : الاسم مالك بن أنس بن مالك (مالك بن أنس بن مالك بن أبي عامر بن عمرو بن الحارث بن غيمان بن خثيل بن عمرو بن الحارث) الكنية: أبو عبد الله النسب: الأصبحي، الحميري، المدني، التيمي، اليمني بلد الإقامة: المدينة علاقات الراوي: حليف عثمان بن عبيد الله القرشي، وكاتبه عيسى بن كنانة وأمه العالية بنت شريك بن عبد الرحمن بن شريك الأزدية، وأخوه النضر، وعمه أبو سهيل نافع بن مالك تاريخ الميلاد: 92 هـ، أو 93، أو 94 هـ، أو 95 هـ تاريخ الوفاة: 178 هـ، أو 179 هـ بلد الميلاد: ذي المروة بلد الوفاة: المدينة بلد الرحلة: مكة، مصر طبقة رواة التقريب: السابعة الرتبة عند ابن حجر: الفقيه، إمام دار الهجرة، رأس المتقنين، وكبير المتثبتين الرتبة عند الذهبي: الإمام
Play Video
Play Video
01:04:06
Mhadhara: محقرات الذنوب 🔴 LIVE | Dhambi Zenye Kudharauliwa Ust Salim Khatib
Mhadhara ulifanyika Dhul Hijjah 20, 1447H Jumamosi Juni 06, 2026 Dhambi Zenye Kudharauliwa محقرات الذنوب Maana ya Dhambi Zenye Kuhakiriwa معنى محقرات الذنوب محقرات الذنوب هي ما لا يبالي المرء به من الذنوب الصغائر Dhambi Zenye Kuhakiriwa ni zile dhambi ambazo kwazo mtu huwa hazijali miongoni mwa dhambi ndogondogo
Play Video
Play Video
54:40
Darsa: نَوَاقِضُ لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهِ 🔴 LIVE DARSA :Utangulizi تَمْهِيد Vitenguzi vya Uislamu
Darsa ilifanyika Dhul Hijjah 19, 1447H Ijumaa Juni 05, 2026 SEHEMU YA PILI Utangulizi تَمْهِيد Vitenguzi vya kalimat -neno laTawhidi نَوَاقِضُ لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهِ Vitenguzi vya Tawhidi نَوَاقِضُ التَّوْحِيد Vitenguzi vya Uislamu نَوَاقِضُ الِإسْلاَم Vitenguzi vya KUMI Uislamu النواقض الِإسْلاَم العشرة Cha Kwanza: Kumshirikisha Allah katika Ibada الأول: الشرك في عبادة الله Cha Pili:Mwenye kuweka baina yake na baina ya Allah mkati na kati الثاني: من جعل بينه وبين الله وسائط الثالث: من لم يكفر المشركين أو شك في كفرهم أو صحح مذهبهم Cha Tatu: Asiyewakufurisha washirikina, au akatilia shaka ukafiri wao au akaonelea kuwa dhehebu lao ni sahihi الرابع: من اعتقد أن هدي غير النبي ﷺ أكمل من هديه، أو أن حكم غيره أحسن من حكمه Cha Nne: Mwenye kuitakidi kwamba uongofu usiokuwa wa Nabii ﷺ ni mkalifu zaid kuliko Uongofu wake ﷺ ; au kwamba hukumu ya ghairi yake ni bora kuliko hukumu yake ﷺ. الخامس: من أبغض شيئاً مما جاء به الرسول ﷺ ولو عمل به Cha Tano:Mwenye kubughudhi kitu chochote kile miongoni mwa yale aliyokuja nayo Rasuli ﷺ na hata kama atakifanya kitu hicho. السادس: من استهزأ بشيء من دين الرسول ﷺ أو ثوابه أو عقابه Cha Sita: Mwenye kufanyia istihzai –mzaha/dhihaki- kitu chochote kile miongoni mwa mambo ya Dini ya Rasuli ﷺ au Thawabu za Allah au Ikabu yake Cha Saba:Sihiri /uchawi السابع: السحر ومنه الصرف والعطف الثامن: مظاهرة المشركين ومعاونتهم على المسلمين Cha Nane: Kuwapa nguvu washirikina na kuwasaidia dhidi ya Waislamu التاسع: من اعتقد أن بعض الناس يسعه الخروج عن شريعة محمد ﷺ Cha Tisa: Mwenye kuitakidi kuwa baadhi ya watu wanaweza kutoka katika Sharia ya Nabii Muhammad ﷺ العاشر: الإعراض عن دين الله لا يتعلمه ولا يعمل به Cha Kumi: Kuipuuza Dini ya Allah; hajifunzi na wala haifanyii kazi.
Play Video
Play Video
01:02:28
Majilisi: عشر ذي الحجة 🔴LIVE DARSA فَضَائِلُ يَوْمِ عَرَفَة Ust Abu Raifah
Majilisi ilifanyika Dhul Hijjah 09, 1447H Jumanne Mei 26, 2026 Fadhila za Siku a Arafah فَضَائِلُ يَوْمِ عَرَفَة Kwa hakika utekelezaji wa ibada ya Hija kwenye Baiti ya Allah ni nguzo katika nguzo tano za Kiislamu, nayo ni wajibu juu ya kila Muislamu aliyebaleghe mwenye akili timamu na mwenye uwezo , kama Alivyosema Allah تَبَارَكَ وَتَعَالَى; ﴾لِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا ۚ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ ﴿٩٧ "Na kwa ajili ya Allah imewajibika juu ya watu kutekeleze (ibada ya) Haji katika nyumba hiyo (Ka’bah) kwa mwenye uwezo; na (yeyote yule) atakayekanusha (hilo), basi hakika Allah ni Ghaniyun –Mkwasi- kwa walimwengu." [Aal Imran 3:97.] Na kumethibiti kwa ajili ya ibada hii adhimu fadhila nyingi; miongoni mwake: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ " الْعُمْرَةُ إِلَى الْعُمْرَةِ كَفَّارَةٌ لِمَا بَيْنَهُمَا، وَالْحَجُّ الْمَبْرُورُ لَيْسَ لَهُ جَزَاءٌ إِلاَّ الْجَنَّةُ ". Kutokana na Abu Hurayrah رضى الله عنه kwamba Rasuli wa Alla صلى الله عليه وسلم amesema: "Umrah hadi Umrah (nyengine) ni kafara (inafuta dhambi) kwa yale yaliyokuwa baina yake (yaani baina Umrah na Umrah nyengine); na Hija Mab-ruru (ni ile Hija iliyotakabaliwa kwa kutimia hukumu zake, na kwa kutochanganyika na dhambi yoyote ile) huwa haina jaza –malipo- isipokuwa Jannah.” Na pia kauli ya Nabii صلى الله عليه وسلم: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " مَنْ حَجَّ هَذَا الْبَيْتَ، فَلَمْ يَرْفُثْ وَلَمْ يَفْسُقْ، رَجَعَ كَمَا وَلَدَتْهُ أُمُّهُ ". Amesimulia Abu Hurayrah رضى الله عنه kuwa Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم amesema: “Yeyote yule atakaetekeleza (ibada ya) Hija (kwenye) hii Baiti (yaani: Al Ka'bah), akawa hakumkaribia (mkewe) kwa ajili ya kufanya tendo la jimai (au kwa yale yote yenye kueleweka kuwa ni vitangulizi vya tendo la jimai; kama kubusiana na mfano wake, na vitangulizi vya kauli; kama vile maneno yenye kufungamana na jimai na matamanio, na pia inajumuisha maneno machafu) na wala hakufanya ufasiki, basi atarudi (kwao baada ya kutekeleza ibada ya Haji) hali ya kuwa (hana dhambi yoyote ile; yaani: yamefutwa) kama alivyozaliwa na mama ake.” Kisha Allah تَعَالَى Akajaalia utekelezaji wa nguzo hii (yaani: ibada ya Hija) uwe ndani ya masiku kumi bora zaidi katika masiku ya mwaka kama alivyosema Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم . عن ابن عمر رضي الله عنهما عن النبي صلى الله عليه وسلم قال” ما من أيام أَعْظَمُ عند الله ولا أَحَبُّ إليه العمل فيهن من هذه الأيام العشر…". Kutokana na Ibn Omar رضي الله عنهما kutokana na Nabiiصلى الله عليه وسلم kuwa amesema: "Hakuna siku zilizo adhimu zaidi mbele ya Allah na wala hakuna amali inayopendeza mno (kufanywa) ndani yake kuliko (ile amali inayofanywa ndani ya) masiku kumi haya (yaani: siku kumi za mwanzo za Shahari ya Dhul Hijjah)…...” Kisha Allah Ta'alaa Akaichagua Yawmu Arafah miongoni mwa masiku kumi haya (yaani: siku kumi za mwanzo za Shahari ya Dhul Hijjah) iwe ni yenye fadhila nyingi, na (pia) Akajaalia kusimama ndani yake (yaani: kisimamo cha Yawmu Arafah) kiwe ndio nguzo ya Hija adhimu; kama alivyosema Nabii صلى الله عليه وسلم : عَنْ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ يَعْمَرَ رضي الله عنه قَالَ شَهِدْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَأَتَاهُ نَاسٌ فَسَأَلُوهُ عَنِ الْحَجِّ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " الْحَجُّ عَرَفَةُ فَمَنْ أَدْرَكَ لَيْلَةَ عَرَفَةَ قَبْلَ طُلُوعِ الْفَجْرِ مِنْ لَيْلَةِ جَمْعٍ فَقَدْ تَمَّ حَجُّهُ " Kutokana na Abdur Rahman bin Ya‘amarرضي الله عنه amesema kuwa nilimshuhudia (yaani: nilimuona) Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم akisema kuwa: "Hija ni (kusimama kisimamo cha Yawmu) Arafah; hivyo basi yeyote yule atakayeweza kuudiriki usiku wa (Yawmu) Arafah kabla ya kuchomoza Alfajiri ya kufikia usiku wa Jam (Muzdalifa), basi kwa hakika Hija yake itakuwa imetimilia (yaani: ameipata Hija).” * Nini sababu ya kuitwa kwa jina hili ما سبب تسميته بهذا الاسم؟ * Siku Bora Kabisa ya Mwaka * Siku ambayo Allah تَعَالَى Alikamilisha Dini na Akatimiza Kwayo Neema * Siku ambayo Kwayo Wengi Huachwa Huru na Moto *Siku Ambayo kwayo Rabi Huwa Karibu na Waja Wake *Siku Ambayo Kwayo Allah Hujigamba na Ahali wa Arafah kwa Malaika *Siku Ambayo Kwayo Allah Huitika Dua ya Ahali wa Arafah *Siku Ambayo Kwayo shetani huwa hakiri zaidi
Contact
bottom of page