top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:02:38
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE باب فضل الغَنِيّ الشاكر Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 21, 1448 H Jumanne Agosti 04, 2026 باب فضل الغَنِيّ الشاكر وهو من أخذ المال من وجهه وصرفه في وجوهه المأمور بِهَا Mlango wa Fadhila/Ubora wa Tajiri mwenye kushukuru na ambae kuchuma Mali na njia itakiwayo (Halali) na kuitumia katika njia Iliyoamriwa kwayo :قَالَ الله تَعَالَى ﴾فَأَمَّا مَنْ أَعْطَىٰ وَاتَّقَىٰ ﴿٥﴾ وَصَدَّقَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٦﴾ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْيُسْرَىٰ ﴿٧ "Basi yule anayetoa (mali) na akamcha Allah. Na akasadikisha Al-Husnaa (jazaa na laa ilaha illallah). Basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo mepesi." [Al-Layl 92:5-7] ﴾وَسَيُجَنَّبُهَا الْأَتْقَى ﴿١٧﴾ الَّذِي يُؤْتِي مَالَهُ يَتَزَكَّىٰ ﴿١٨﴾ وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُ مِن نِّعْمَةٍ تُجْزَىٰ ﴿١٩﴾ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٠ ﴾وَلَسَوْفَ يَرْضَىٰ ﴿٢١ "Na ataepushwa nao mwenye taqwa kabisa. Ambaye anatoa mali yake kujitakasa. Na hali hakuna mmoja yeyote aliyemfanyia fadhila yoyote hata amlipe. Isipokuwa kutaka Wajihi wa Rabi wake Aliyetukuka. Na bila shaka atakuja kuridhika." [Al-Layl 92:17-21] ﴾إِن تُبْدُوا الصَّدَقَاتِ فَنِعِمَّا هِيَ ۖ وَإِن تُخْفُوهَا وَتُؤْتُوهَا الْفُقَرَاءَ فَهُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۚ وَيُكَفِّرُ عَنكُم مِّن سَيِّئَاتِكُمْ ۗ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴿٢٧١ "Mkidhihirisha Sadaka basi ni vizuri hivyo, na mkizificha na kuwapa mafakiri, basi hilo ni heri kwenu; na Atakufutieni katika maovu yenu; na Allah kwa yale myatendayo, ni Khabir (Mwenye upeo wa habari za dhahiri na za batini.)" [Al-Baqarah 2:271] ﴾لَن تَنَالُوا الْبِرَّ حَتَّىٰ تُنفِقُوا مِمَّا تُحِبُّونَ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِن شَيْءٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٩٢ "Hamtoweza kuufikia wema mpaka mtoe katika vile mnavyovipenda; na kitu chochote mnachotoa basi hakika Allah kwacho ni Alimu (Mjuzi)." [Aal-'Imraan 3:92]
Play Video
Play Video
01:02:52
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴LIVE باب الإيثار والمواساة Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 20, 1448 H Jumatatu Agosti 03, 2026 Mlango wa Kupendelea wengine na kusaidiana باب الإيثار والمواساة :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ ﴿٩ "Na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wanahitaji." [Al-Hashr 59:9] ﴾وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا ﴿٨ "Na wanalisha chakula juu ya kukipenda kwao, masikini na mayatima na mateka." [Al-Insan 76:8] باب التنافس في أمور الآخرة والاستكثار مما يتبرك بِهِ Mlango wa Kushindana Katika Mambo Yanayohusu Akhera na Kukithirisha (kutaka) Vitu vya Baraka :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ ﴿٢٦ "Na katika hayo basi washindane wenye kushindana. "[Al-Mutwaffifina 83: 26]
Play Video
Play Video
01:16:12
Mhadhara: أهمية القرآن العظيم في حياة المسلم 🔴 LIVE | Ust Badr S Ja'far kutoka Nairobi, Kenya
Darsa ilifanyika Swafar 18, 1448 H Jumamosi Agosti 01, 2026 أهمية القرآن العظيم في حياة المسلم اليومية Umuhimu wa Qur aani katika Maisha ya Muislamu ya kila Siku :قال تعالى ﴾إِنَّ هَـٰذَا الْقُرْآنَ يَهْدِي لِلَّتِي هِيَ أَقْوَمُ وَيُبَشِّرُ الْمُؤْمِنِينَ الَّذِينَ يَعْمَلُونَ الصَّالِحَاتِ أَنَّ لَهُمْ أَجْرًا كَبِيرًا ﴿٩ "Hakika hii Qur aani inaongoza katika yaliyonyooka kabisa, na inawabashiria Waumini wanaotenda mema kwamba watapata ujira mkubwa." [Al Is-raa 17:9.] Umuhimu wa Qur aani unatokana na yale yaliyokusanyika ndani yake katika kuelekeza na kutoa uongofu/mwongozo katika itikadi sahihi, na mambo ya ibada za hali na kweli, na maadili mema na tabia njema, na miamalati na sharia za kiadilifu na haki, pamoja na mafundisho yake ya kujenga jamii yenye maadili mema na kuimarisha dola imara. Iwapo Waislamu watajadidi imani yao juu ya umuhimu wa Qur aani tukufu katika maisha yao, na wakawa makini katika kushikamana na kufuata bali kutii Amri na Maagizo/maelekezo ya Kiungu yenye hekima yaliyomo ndani ya Qur aani; kwani wanapata kile wanachohitaji kutoka katika maisha ya kiroho yaliyosafi, na nguvu za kisiasa na kijeshi, utajiri na ustaarabu, pamoja na neema na baraka zisizohesabika. :قال تعالى ﴾وَلَوْ أَنَّ أَهْلَ الْقُرَىٰ آمَنُوا وَاتَّقَوْا لَفَتَحْنَا عَلَيْهِم بَرَكَاتٍ مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ وَلَـٰكِن كَذَّبُوا فَأَخَذْنَاهُم بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ ﴿٩٦ "Na lau kama watu wa miji wangeliamimi na (wakashikamana na) taqwa, kwa yakini Tungeliwafungulia baraka nyingi kutoka mbinguni na ardhini, walakini walikadhibisha; basi Tuliwachukua (Tuliwaadhibu/Tuliwaangamiza) kwa sababu ya yale waliyokuwa wakiyachuma." [Al A'raaf 7:96] Ikiwa Waislamu wanataka heri, na kutengamaa na utukufu, na heshima kwa ajili ya nafsi zao wenyewe na kwa ajili ya umma wao, basi ni juu yao kuifuata Qur aani Takatifu katika maisha yao ya kila siku kulingana na mwongozo wa Mtume Muhammad صلّى الله عليه وسلّم na Swahaba zake رضي الله عنهم na kuhakikisha kuwa wanaipa Qur aani nafasi, na hadhi na heshima yake iliyopewa na Allah na Rasuli Wake صلّى الله عليه وسلّم kwa kuyatekeleza na kuyafanyia kazi maamrisho na maagizo yake na kujikataza kwa kujiweka mbali na makatazo yake. لن يصلح آخر هذه الأمة إلا بما صلح به أوّلها Kwani hakuna njia wala uwezekano wa kutengamaa na wala kufanikiwa na kufaulu wa mwisho wa umma huu isipokuwa kwa kilekile kilichopelekea kutengemaa, kufanikiwa na kufaulu wa mwanzo wake.
Play Video
Play Video
01:03:15
Darsa: (VII) الشرك في عبادة الله 🔴 اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ
Darsa ilifanyika Swafar 17, 1448 H Ijumaa Julai 31, 2026 SEHEMU YA SABA Utangulizi تَمْهِيد Vitenguzi vya kalimat -neno laTawhidi نَوَاقِضُ لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهِ Vitenguzi vya Tawhidi نَوَاقِضُ التَّوْحِيد Vitenguzi vya Uislamu نَوَاقِضُ الِإسْلاَم اعْلَمْ أنَّ مِنْ أَعْظَمِ نَوَاقِضِ الإِسْلَامِ عَشْرَةَ Elewa kwamba katika vitenguzi VIKUBWA kabisa vya Uislamu ni mambo KUMI. Elewa na tambua na uwe na yakini ya kwamba Uislamu wa mtu unatenguka kwa kufanya moja lolote lile miongoni mwa mambo kumi yenye kutengua Uislamu. Vitenguzi vya KUMI Uislamu النواقض الِإسْلاَم العشرة Kitenguzi cha Kwanza: Kumshirikisha Allah katika Ibada الأول: الشرك في عبادة الله
Play Video
Play Video
01:10:12
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE باب: النهي عن البخل والشح Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 15, 1448 H Jumatano Julai 29, 2026 Mlango wa kukatazwa Ubahili na Uchoyo باب: النهي عن البخل والشح :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَأَمَّا مَن بَخِلَ وَاسْتَغْنَىٰ ﴿٨﴾ وَكَذَّبَ بِالْحُسْنَىٰ ﴿٩﴾ فَسَنُيَسِّرُهُ لِلْعُسْرَىٰ ﴿١٠﴾ وَمَا يُغْنِي عَنْهُ مَالُهُ إِذَا تَرَدَّىٰ ﴿١١ "Ama yule afanyaye ubahili na akajiona amejitosheleza. Na akakadhibisha Al-Husnaa (anayowajibika kuyasadiki). Basi Tutamuwepesishia kwa yaliyo magumu. Na itamsaidia nini mali yake atakapoporomoka kuangamia (Motoni)." Al-Layl 92: 8-11] ﴾وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ﴿١٦ "Na yeyote yule anayeepushwa na ubahili na tamaa ya uchu wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu." [At-Taghaabun 64:16] Hadithi – 1 : وعن جابر رضي الله عنه أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ اتَّقُوا الظُّلْمَ ؛ فَإِنَّ الظُّلْمَ ظُلُمَاتٌ يَوْمَ القِيَامَةِ . وَاتَّقُوا الشُّحَّ ؛" ". فَإنَّ الشُّحَّ أهْلَكَ مَنْ كَانَ قَبْلَكُمْ ، حَمَلَهُمْ عَلَى أنْ سَفَكُوا دِمَاءهُمْ وَاسْتَحَلُّوا مَحَارِمَهُمْ رواه مسلم Imepokewa kutoka kwa Jabir رضي الله عنه kwamba Rasuli wa Allah صلى الله عليه وسلم amesema: "Ogopeni dhulma, kwani hakika dhulma ni viza (kwa mwenye kuifanya) Siku ya Qiyaamah; na ogopeni (tahadharini) na ubahili, kwani hakika ubahili (ndio) uliowahilikisha -waangamiza- waliokuwa kabla yenu; huu (ubahili ndio) uliwapelekea wao kumwaga damu na kuhalalisha vilivyo haramu." Muslim Mlango wa Kupendelea wengine na kusaidiana باب الإيثار والمواساة :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَيُؤْثِرُونَ عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ وَلَوْ كَانَ بِهِمْ خَصَاصَةٌ ۚ ﴿٩ "Na wanawapendelea kuliko nafsi zao japokuwa wao wenyewe wanahitaji." [Al-Hashr 59:9] ﴾وَيُطْعِمُونَ الطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِ مِسْكِينًا وَيَتِيمًا وَأَسِيرًا ﴿٨ "Na wanalisha chakula juu ya kukipenda kwao, masikini na mayatima na mateka." [Al-Insan 76:8]
Play Video
Play Video
51:32
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE (IV) باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 14, 1448 H Jumanne Julai 28, 2026 باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير ثقةً بالله تعالى Mlango wa ukarimu na kutoa katika njia za heri na kuwa na matumaini na Allah تعالى SEHEMU YA NNE :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ۖ ﴿٣٩ "Na kitu chochote mtoacho, basi Yeye Atakilipa..". [Sabaa 34: 39] ﴾وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَلِأَنفُسِكُمْ ۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ اللَّـهِ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ ﴿٢٧٢ "Na chochote cha heri mtoacho basi ni kwa ajili ya nafsi zenu; na hamtoi isipokuwa kutaka Wajhi wa Allah; na chochote mtoacho katika heri mtalipwa kamilifu nanyi hamtodhulumiwa." [Al-Baqarah 2: 272] ﴾ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣ "Na chochote mtoacho katika heri basi Allah kwacho ni Alimu (Mjuzi)." [Al-Baqarah 2:273]
Play Video
Play Video
01:01:33
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات🔴LIVE (III) باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير Sh Salim
Darsa ilifanyika Swafar 13, 1448 H Jumatatu Julai 27, 2026 باب الكرم والجود والإنفاق في وجوه الخير ثقةً بالله تعالى Mlango wa ukarimu na kutoa katika njia za heri na kuwa na matumaini na Allah تعالى SEHEMU YA TATU :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَمَا أَنفَقْتُم مِّن شَيْءٍ فَهُوَ يُخْلِفُهُ ۖ ﴿٣٩ "Na kitu chochote mtoacho, basi Yeye Atakilipa..". [Sabaa 34: 39] ﴾وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَلِأَنفُسِكُمْ ۚ وَمَا تُنفِقُونَ إِلَّا ابْتِغَاءَ وَجْهِ اللَّـهِ ۚ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ يُوَفَّ إِلَيْكُمْ وَأَنتُمْ لَا تُظْلَمُونَ ﴿٢٧٢ "Na chochote cha heri mtoacho basi ni kwa ajili ya nafsi zenu; na hamtoi isipokuwa kutaka Wajhi wa Allah; na chochote mtoacho katika heri mtalipwa kamilifu nanyi hamtodhulumiwa." [Al-Baqarah 2: 272] ﴾ وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣ "Na chochote mtoacho katika heri basi Allah kwacho ni Alimu (Mjuzi)." [Al-Baqarah 2:273]
Play Video
Play Video
40:42
Darsa: Mirathi:أَقْسَامُ الوَرَثَةِ بِاعْتِبَارِالإِرْثِ 🔴 LIVE UMMU أُمٌّ (II) Dr. Ibrahim Bulushi
Darsa ilifanyika Swafar 11, 1448H Jumamosi Julai 25, 2026 أَقْسَامُ الوَرَثَةِ بِاعْتِبَارِالإِرْثِ َMakundi (vigawanyo) vya Warithi kwa kuzingatia (namna za) KURITHI KUNDI LA KWANZA Wenye Kurithi kwa FAR-DHU PEKEE من يَرِثُ بِالْفَرْضِ فَقَط Warithi wenye kustahiki kurithi kwa FAR DHU PEKEE ni SABA (7) 1. UMMU أُمٌّ 2. MUME الزَّوْجُ 3. MKE زوْجَةٌ 4. BIBI (NYANYA) KWA MAMA جَدَّةٌ 5. BIBI (NYANYA) KWA BABA جَدَّةٌ 6. AKH KWA MAMA MMOJA الأخُ لأمِّ 7. UKHTI KWA MAMA MMOJA الأُخْت لأمّ Mrithi wa kwanza mwenye kustahiki kurithi kwa FAR DHU PEKEE MAMA/UMMU أُمٌّ UMMU hustahiki kurithi FAR DHU TATU (3) PEKEE: 1. SUDUSI (1/6) السُّدُسُ 2. THELUTHI (1/3) الثُّلُثُ 3. THELUTHI ILIYOBAKI ثلث الباقي UMMU/MAMA HUSTAHIKI KURITHI KWA FAR DHU KATIKA HALI NNE (4): HALI YA KWANZA ﴾وَلِأَبَوَيْهِ لِكُلِّ وَاحِدٍ مِّنْهُمَا السُّدُسُ مِمَّا تَرَكَ إِن كَانَ لَهُ وَلَدٌ ﴿١١ “Na WAZAZI WAKE WAWILI (UMMU/MAMA NI MMOJA WA HAO WAZAZI WAWILI) kila mmoja wao atastahiki SUDUSI (1/6) katika alichoacha (MRITHIEWA) IKIWA (MRITHIWA) ANA WALAD ....” [An Nisaa 4:11] HALI YA PILI : ﴾فَإِن كَانَ لَهُ إِخْوَةٌ فَلِأُمِّهِ السُّدُسُ ۚ ﴿١١ "Na ikiwa (mrithiwa) ana Ikhwah (yaani: ndugu: wa kike au wa kiume) basi UMMU/MAMA wake atastahiki SUDUSI (1/6) ..” [An Nisaa 4:11] HALI YA TATU: ﴾وَوَرِثَهُ أَبَوَاهُ فَلِأُمِّهِ الثُّلُثُ ۚ ﴿١١ “Na (ikiwa) WAZAZI WAKE WAWILI NDIO WARITHI WAKE (MRITHIWA: YAANI HAKUNA MRITHI ISIPOKUWA WAZAZI WAWILI PEKEE), BASI UMMU/MAMA YAKE ATASTAHIKI THELUTHI (1/3)..” [An Nisaa 4:11] HALI YA NNE: مسألة العمريتين MAS-ALA ZENYE KUELEWEKA KWA JINA LA: AL UMARIYYATAYNI AMBAYO YAKO NA HALI MBILI
Contact
bottom of page