top of page
Darsa Na Mihadhara
Home
Kuhusu Sisi
Vitabu
Mwongozo wa kujiandaa na ibada ya Umrah
Aina za watu wanaokwenda kutekeleza Ibada ya Umrah
Fadhila za siku kumi za Dhul Hijjah
Itikadi Ya Maimamu Wane
Videos
Makala
Mafundisho
Aqidah
Qur'aan
Fiqh
Sira
Khutbah
Contact
About
More
Use tab to navigate through the menu items.
Log In
Darsa
na Mihadhara Online
ٱقْرَأْ بِٱسْمِ رَبِّكَ ٱلَّذِى خَلَقَ
Soma kwa ajili ya Mola wako aliyeumba
Al-Alaq 91;1
Darsa na Mihadhara
Play Video
Play Video
01:01:39
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE DARSA (II) حسن الخلق Sh Salim
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 27, 1448 H Jumatano Septemba 09, 2026 SEHEMU YA PILI Mlango Wa Tabia Njema باب حسن الخلق :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤ "Na hakika wewe uko juu ya kiwango adhimu cha akhalaqi njema." [Al-Qalam 68:4] ﴾ وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ ﴿١٣٤ "Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu." [Aal-'Imraan 3:134]
Play Video
Play Video
58:48
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE DARSA (I) حسن الخلق Sh Salim
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 26, 1448 H Jumanne Septemba 08, 2026 SEHEMU YA KWANZA Mlango Wa Tabia Njema باب حسن الخلق :قَالَ الله تَعَالَى ﴾وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤ "Na hakika wewe uko juu ya kiwango adhimu cha akhalaqi njema." [Al-Qalam 68:4] ﴾ وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ ۗ ﴿١٣٤ "Na wanazuia ghadhabu, na wenye kusamehe watu." [Aal-'Imraan 3:134]
Play Video
Play Video
01:07:24
Darsa ya Riyaadhu كِتابُ الْمُقَدِّمات 🔴 LIVE DARSA (II) باب تحريم الكبر والإعجاب Sh Salim
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 25, 1448 H Jumatatu Septemba 07, 2026 SEHEMU YA PILI Mlango wa Kuharamishwa Kiburi na Kujiona باب تحريم الكبر والإعجاب :قَالَ الله تَعَالَى ﴾تِلْكَ الدَّارُ الْآخِرَةُ نَجْعَلُهَا لِلَّذِينَ لَا يُرِيدُونَ عُلُوًّا فِي الْأَرْضِ وَلَا فَسَادًا ۚ وَالْعَاقِبَةُ لِلْمُتَّقِينَ ﴿٨٣ "Hiyo ni nyumba ya Akhera, Tunaijaalia kwa wale wasiotaka kujitukuza katika ardhi na wala ufisadi; na hatima njema ni kwa wenye taqwa." [Al-Qaswasw : 83] ﴾وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ ﴿٣٧ "Na wala usitembee katika ardhi kwa majivuno." [Al-Israa: 37] ﴾وَلَا تُصَعِّرْ خَدَّكَ لِلنَّاسِ وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ كُلَّ مُخْتَالٍ فَخُورٍ ﴿١٨ "Na wala usiwageuzie watu uso wako kwa kiburi, na wala usitembee katika ardhi kwa maringo, hakika Allah Hampendi kila mwenye kujivuna mwenye kujifakharisha." [Luqmaan: 18] إِنَّ قَارُونَ كَانَ مِن قَوْمِ مُوسَىٰ فَبَغَىٰ عَلَيْهِمْ ۖ وَآتَيْنَاهُ مِنَ الْكُنُوزِ مَا إِنَّ مَفَاتِحَهُ لَتَنُوءُ بِالْعُصْبَةِ أُولِي الْقُوَّةِ ﴾إِذْ قَالَ لَهُ قَوْمُهُ لَا تَفْرَحْ ۖ إِنَّ اللَّـهَ لَا يُحِبُّ الْفَرِحِينَ ﴿٧٦ "Hakika Qaaruna alikuwa miongoni mwa kaumu ya Musa, walakini aliwafanyia uonevu kwa kutakabari; na Tulimpa katika hazina ambazo funguo zake zinalemea kundi la watu wenye nguvu (kuzibeba); (kumbuka pale) walipomwambia watu wake: Usifurahi kwa kujigamba; hakika Allah Hapendi wanaofurahi kwa kujigamba." [Al-Qaswasw: 76] ﴾فَخَسَفْنَا بِهِ وَبِدَارِهِ الْأَرْضَ ﴿٨١ "Basi Tukamdidimiza yeye na nyumba yake ardhini" [Al-Qaswasw: 81]
Play Video
Play Video
02:08:33
Darsa:أَرْبَعَةُ أَسْبَابٍ خَفِيَّةٍ لِهَلَاكِ الأَبْنَاءِ 🔴DARSA:(II) Maangamizi Manne Ust. Hassan
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 24, 1448 H Jumapili Septemba 06, 2026 SEHEMU YA PILI أَرْبَعَةُ أَسْبَابٍ خَفِيَّةٍ لِهَلَاكِ الأَبْنَاءِ ــ أخْطَاءٌ يَرْتَكِبُهَا آبَاءُ القَرْنِ ٢١ ضِدَّ أَجْيَالِهِمْ Maangamizi Manne Hatari Yaliyojificha: Makosa ya Wazazi wa Karne ya 21 Yanaoharibu Kizazi
Play Video
Play Video
01:03:55
DARSA:الجامع لعبادة الله وحده🔴DARSA:Kurejea kwa Allah الإنابة na Mahaba المَحَبَّة Ust Bin Masoud
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 24, 1448 H Jumapili Septemba 06, 2026 الجامع لعبادة الله وحده Al Jaami'u (Kusanyo lenye Kuhusiana na) Ibada kwa Ajili ya Allah Pekee Kutarajia/Tarajia (kuwa na matumaini ya kupata heri) والرجاء Tawakali (Kutawakali/kutegemea) والتوكل Kurejea kwa Allah الإنابة ﴾وَأَنِيبُوا إِلَىٰ رَبِّكُمْ وَأَسْلِمُوا لَهُ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَكُمُ الْعَذَابُ ثُمَّ لَا تُنصَرُونَ﴿٥٤ "Na rudini kwa Rabi wenu (kwa kutubu na kufanya mema) na jisalimisheni Kwake kabla haijakufikieni adhabu, kisha hamtonusuriwa." [Az Zumar 39:45] Mahaba المَحَبَّة
Play Video
Play Video
50:21
DARSA: الجامع لعبادة الله وحده 🔴DARSA: Kutarajia والرجاء na Kutawakali والتوكل. Ust Ali bin Masoud
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 23, 1448 H Jumamosi Septemba 05, 2026 الجامع لعبادة الله وحده Al Jaami'u (Kusanyo lenye Kuhusiana na) Ibada kwa Ajili ya Allah Pekee Kutarajia/Tarajia (kuwa na matumaini ya kupata heri) والرجاء من أنواع العبادة الرجاء : وهو تأميل الخير فيما لا يقدر عليه إلا الله Katika aina za ibada ni Kutarajia: nako ni kutarajia heri (yaani:kuwa na matumaini ya kupata heri) katika yale mambo ambayo kwayo hakuna ayawezae mambo hayo isipokuwa Allah Pekee. فلا يجوز أن ترجو غير الله فيما لا يقدر عليه إلا الله Hivyo basi haijuzu -hairuhusiwi- kumtumainia yeyote mwengine isiyekuwa Allah katika yale mambo ambayo hakuna ayawezae isipokuwa Allah Pekee. Ama kuhusiana na kumtarajia mtu katika mambo ya kawaida أما الرجاء في الأمور العادية كأن ترجو من شخص أن يعطيك مالاً أو يساعدك فيما يقدر عليه kama vile kutarajia kwamba mtu atakupa mali au kukusaidia katika yale ambayo anayaweza kufanya; hii halina ubaya kwa kuwa si katika Ibada فهذا ليس من العبادة تقول : يا أخي، أرجوك أن تعطيني كذا وكذا، مما يقدر عليه Unaweza kusema: Ewe ndugu yangu! nakuomba unipe kadha na kadha, ukimaanisha katika yale mambo ambayo anayaweza kufanya. لكن لا ترج مخلوقا فيما لا يقدر عليه إلا الله walakini usimtarajie mahuluku yoyote yule katika yale ambayo hakuna ayawezae isipokuwa Allah Pekee. كالذين يرجون الأموات والغائبين والجن، هذا يجوز، وهو شرك أكبر Kama wale wanaowatarajia -wenye kuweka matumaini yao- wafu, na wasiokuwepo, na majini; hili halijuzu -haliruhusiwa- nalo ni shirki kubwa. Tawakali (Kutawakali/kutegemea) والتوكل من أنواع العبادة التوكل : وهو تفويض الأمور إلى الله الاعتماد عليه Tawakali ni katika aina za Ibada nako ni kuyafawidhi mambo yote kwa Allah kumtegemea ambayo ni kumkabidhi Mungu mambo na kumtegemea. Amesema Ibn Rajab katika kufafanua Tawakati :قال ابن رجب في تعريف التوكل هو صدق اعتماد القلب على الله عز وجل في استجلاب المصالح Tawakuli ni: ukweli wa muegemeo -uwegemeaji- wa moyo kuegemea kwa Allah katika kuleta mambo yenye maslahi na manufaa. ودفع المضار من أمور الدنيا والآخرة كلها Na kuepusha -kujikinga na- madhara katika mambo ya kidunia na Akhera وكِلَةُ الأمور كلها إليه Na kuyaegemeza mambo yote Kwake (yaani: Allah Pekee) وتحقيق الإيمان بأنه لا يعطي ولا يمنع ولا يضر ولا ينفع سواه Na kuhakiki -kuthibitisha- imani kwamba hakuna yeyote yule anaeweza kutoa na wala anaeweza kuzuia na wala anaeweza kudhuru na wala anaeweza kunufaisha isipokuwa Yeye (yaani: Allah Pekee). ﴾عَلَى اللَّـهِ فَتَوَكَّلُوا إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ ﴿٢٣ "Na kwa Allah Pekee tawakalini ikiwa nyinyi ni Waumini (wa kwelikweli)." [Al Maaidah 5:23] ﴾فَاعْبُدْهُ وَتَوَكَّلْ عَلَيْهِ ۚ ﴿١٢٣ "basi muabudu Yeye Pekee, na tawakali Kwake ...." [Huud 11:123] Kutawakali ni ibada; haijuzu isipokuwa kwa Mungu. فالتوكل عبادة لا يجوز إلا الله أما التوكيل فيما يقدر عليه المخلوق، كأن توكل أحدا يشتري لك حاجة Ama kuhusiana na kuteua atakaewakilisha katika yale anayoyaweza mahuluku, kama vile kumteua mmoja yeyote yule akununulie kitu. وتوكل أحدا يعمل لك عملا، هذا جائز Na unaweza kumteua mtu wa akuwakilishe kwa (kukufanyia) kazi; hii inajuzu (inaruhusiwa). ﴾فَابْعَثُوا أَحَدَكُم بِوَرِقِكُمْ هَـٰذِهِ إِلَى الْمَدِينَةِ فَلْيَنظُرْ أَيُّهَا أَزْكَىٰ طَعَامًا فَلْيَأْتِكُم بِرِزْقٍ مِّنْهُ وَلْيَتَلَطَّفْ وَلَا يُشْعِرَنَّ بِكُمْ أَحَدًا ﴿١٩ "Basi tumeni mmoja wenu mjini kwa noti zenu hizi atazame chakula chake kipi kifaacho zaidi kisha akuleteeni chakula hicho; na awe makini na busara, na wala asikutambulisheni kwa mmoja yeyote yule."[Al Kahf 18:19]. Huu (kwenye Aayah) ni uwakilishaji, na uwakilishaji unaruhusiwa هذا توكيل، فالتوكيل جائز Ama kutawakali huwa inamuhusu (yaani:hasa kwa) Allah Pekee أما التوكل فإنه خاصا بالله
Play Video
Play Video
01:04:54
DARSA: الرسول صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآله وسَلَّمَ في المَدِينةِ 🔴LIVE|DARSA وثيقة المدينة Ust Salim
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 22, 1448 H Ijumaa Septemba 04, 2026 Utangulizi المقدمة SEHEMU YA KWANZA Rasuli صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآله وسَلَّمَ akiwa Madina الرسول صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآله وسَلَّمَ في المَدِينةِ Hati (Sahifa/Katiba/Desturi) ya Madina وثيقة المدينة صحيفةُ المدينة أول وثيقة دستورية في التاريخ الإسلامي Hati/Sahifa ya Madina ndiyo hati ya kwanza ya kikatiba katika historia ya Kiislamu. وضعها النبي صلى الله عليه وسلم بعد الهجرة Nabii صلى الله عليه وسلم aliiweka hati (katiba) hiyo baada ya Hijra. لتنظيم العلاقات بين سكان المدينة من المسلمين واليهود والوثنيين Kwa gharadhi ya kudhibiti uhusiano baina ya wakaazi wa Madina waliokuwa kwenye makundi: Waislamu Mayahudi Wapagani. فجسدت هذه الوثيقة مبدأ المواطنة والتعايش السلمي Hati hii ilijumuisha kanuni za uraia na kuishi pamoja kwa amani. وأرست أسس العدالة والوحدة في الدولة الناشئة Na ikaiweka misingi madhubuti ya uadilifu na ya umoja katika Dola mpya na changa.
Play Video
Play Video
01:15:10
DARSA: الجامع لعبادة الله وحده 🔴DARSA:Kuomba Uwokovu الاستغاثة, Nadhiri النذر, na Kuogopa الخوف
Darsa ilifanyika Rabi'ul Awwal 22, 1448 H Ijumaa Septemba 04, 2026 الجامع لعبادة الله وحده Al Jaami'u (Kusanyo lenye Kuhusiana na) Ibada kwa Ajili ya Allah Pekee Kanuni Kamili za Kumuabudu Allah Pekee فإن قيل : فما الجامع لعبادة الله وحده؟ Aina za Ibada ni nyingi, kubwa yao ni Dua أنواع العبادة كثيرة أعظمها : الدعاء Kuomba/kutaka/kutafuta msaada الاستعانة Kutafuta uwokovu الاستغاثة Nadhiri النذر النذر : هو التزام عبادة لم يلزم بها الشرع، وهو نوع من أنواع العبادة Nadhiri ni: Kujilazimisha (kufanya) ibada ambayo kwayo Sharia haikuilazimisha; nayo (yaani: hiyo Nadhiri ni) aina miongoni mwa aina za ibada. : قال تعالى ﴾يُوفُونَ بِالنَّذْرِ وَيَخَافُونَ يَوْمًا كَانَ شَرُّهُ مُسْتَطِيرًا﴿٧ "Wanatimiza -wanatekeleza- nadhiri na wanaiogopa Siku ambayo shari yake ni yenye kuenea" [Al Insani 76:7]. Allah Amewasifu kwamba wao wanatimiza nadhiri zao فأثنى عليهم أنهم يوفون بالنذر ﴾وَمَا أَنفَقْتُم مِّن نَّفَقَةٍ أَوْ نَذَرْتُم مِّن نَّذْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُهُ ۗ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَارٍ ﴿٢٧٠ "Na chochote mtoacho au mkiwekacho nadhiri, basi hakika Allah Anakijua; na madhalimu hawana wa kuwanusuru." [Al Baqarah 2:270] قرنه مع النفقة والصدقة، والنفقة والصدقة عبادة، فيكون النذر عبادة Ameifungamanisha (Nadhiri) na Utowaji na Sadaka, na Utowaji na Sadaka ni Ibada, hivyo basi Nadhiri nayo inakuwa ni (kitendo cha) ibada (pia). ﴾وَلْيُوفُوا نُذُورَهُمْ وَلْيَطَّوَّفُوا بِالْبَيْتِ الْعَتِيقِ ﴿٢٩ "watimize -watekeleze- nadhiri zao, na watufu kwenye Baiti ya Kale" [Al-Hajj 22:29]. قرنه مع لطواف، والطواف عبادة لله عز وجلا، فالوفاء بالنذر عبادة، هذا في نذر الطاعة Ameifungamanisha pamoja na kutufu, na kutufu ni (kitendo cha) ibada kwa minajili ya Allah عز وجلا, hivyo basi kutimiza -kutekeleza- Nadhiri ibada, hii inahusiana na Nadhiri za utiifu. إذا نذر أن يتصدق، وإذا نذر أن يصلي، وإذا نذر أن يصوم ، وإذا نذر أن يحج، وإذا نذر أن يعتمر Hivyo basi pale atakapoweka Nadhiri ya kutoa Sadaka, na atakapoweka Nadhiri ya kusali, na atakapoweka Nadhiri ya kufunga, na atakapoweka Nadhiri ya kuhiji, na atakapoweka Nadhiri ya kufanya Umrah; hutakiwa kuzitimiza -kuzitekeleza- kwa kuwa ni Ibada. قال رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " مَنْ نَذَرَ أَنْ يُطِيعَ اللَّهَ فَلْيُطِعْهُ .... " . Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mwenye kuweka nadhiri kwamba atamtii Allah, basi amtii ....” Bukhari, katika Kitabu cha Viapo na Nadhiri, mlango wa Nadhiri ya utiifu. Hadithi namba (6696). Ama zile Nadhiri za maasi, ni haramu kuzitimiza kwake أما نذر المعصية فإنه يحرم الوفاء به قال رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم " وَمَنْ نَذَرَ أَنْ يَعْصِيَ اللَّهَ فَلاَ يَعْصِهِ " . Rasuli wa Allah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: " Na mwenye kuweka nadhiri kwamba atamuasi Allah, basi asimuasi.” Bukhari, katika Kitabu cha Viapo na Nadhiri, , mlango wa Nadhiri ya utiifu.Hadithi namba (6696). Miongoni mwa Nadhiri za Maasi :ومن نذر المعصية النذر للقبور، فمن نذر لقبر أو نذر لميت فإنه يكون مشركا شركا أكبر؛لأنه صرف نوعا من أنواع العبادة لغير الله Kuweka Nadhiri kwa minajili ya makaburi, hivyo basi yeyote yule ataeweka nadhiri kwa minajili ya kaburi au kwa minajili ya maiti, kwa hakika huwa ni mwenye kushirikisha -mshirikina-; shirki kubwa; kwa kuwa ameelekeza aina moja miongoni mwa aina za ibada kwa ghairi -asiyekuwa- Allah عز وجلا. Hofu (Kuogopa) الخوف الخوف من أعمال القلوب، فهو عبادة قلبية Hofu ni miongoni mwa amali za moyo, hivyo basi ni ibada ya kimoyo. والمراد خوف العبادة، هو الخوف الذي يكون معه تعظيم ومحبة للمخوف Muradi -kusudio la- Hofu ya ibada, ni hofu ambayo inakuwa pamoja nayo (yaani: inayoambatana na) kuadhimisha na mahaba kwa Yule anaeogopwa يُحبه ويَخافه، هذا خوف العبادة ويسمى خوف السر، وهو لا يَجُوز إلا الله Anampenda na anamuogopa; hii ndio Hofu ya Ibada, pia huitwa hofu ya siri; na aina hii ya hofu -kuogopa- haijuzu isipokuwa kwa (kumuhofu) Allah Pekee.
Contact
bottom of page